Quantcast
Channel: Makala – ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 676

Jicho la 3: Sababu 4 muhimu ambazo zinawabeba Yanga kuelekea taji la 3 mfululizo VPL

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

MICHEZO  kumi  kuelekea  mwisho  wa  msimu  wa ligi kuu Tanzania bara 2016/17  mabingwa  watetezi  Yanga  SC  wamerejea  katika kilele  cha msimamo  wakiwa na alama  46  baada  ya kucheza  game 20.

Kikosi  cha  Mzambia, George  Lwandamina  na  wasaidizi  wake  Juma Mwambusi  na kocha  wa makipa  Juma  Pondamali  kitacheza  na  Stand United  siku  ya Kesho  Ijumaa na ushindi  uwafanya  watengeneze  gepu  la pointi  nne  zaidi  dhidi  ya  wapinzani  wao  wa  karibu  Simba SC  ambao watacheza na Majimaji  FC  siku  ya  Jumamosi  katika  uwanja  wa Majimaji, Songea.

Kuna  wakati  hata  mashabiki  wa Yanga  walikata tama baada  ya timu  yao  kupoteza  2-1  vs  Mbeya  City FC  mwezi  Novemba (kikiwa ni kipigo  chao  cha  pili  msimu  huu  baada  ya  awali  kufungwa 1-0  na Stand  United).

Lakini  tangu  hapo  kikosi  hicho  kimefanikiwa  kushinda michezo sita  kati  ya Saba iliyopita  na  jambo  hilo  limerejesha  matumaini  makubwa  kuwa  huenda  wakafikia  malengo  yao  ya  kushinda  taji  la tatu  mfululizo.

Baada  ya  kufungwa na City  Novemba 2   niliandika  ili  Yanga  wafikie  malengo  yao  wanapaswa  kuhakikisha  hawapotezi  mchezo mwingine,  pia  nilikumbusha kuhusu ‘tabia  yao’  ya  kutoka  chini  ya  msimamo  na  kushinda  ubingwa  inapaswa  kurejea.  Nakiamini  kikosi  cha Yanga  na ninakichukulia  kuwa ni  kikosi  bora  kuliko  vyote  katika ligi ya Tanzania bara.

Ukiachana  na  historia  yao  ya nyuma  naamini  Yanga  ina  kila  sababu  ya  kushinda  ubingwa  wa VPL  msimu  huu  hasa  baada  ya  kuyumba  kwa Azam FC. Yanga  inabebwa  na  vitu  vingi ambavyo  klabu nyingine  hazina. Ukiachana  na  wingi  wa  mashabiki  wao,  hizi  ni  sababu  nyingine  ambazo ‘Jicho langu  la Tatu’ linaona  zinaibeba  Yanga.

KIKOSI CHENYE WACHEZAJI BORA WAZOEFU NA CHIPUKIZI

Kati  ya  mambo  mazuri  ambayo  Yanga  inanufaika  nayo  hivi  sasa ni kukubali  kumuachia  mwalimu  aliyepita  Mholland, Hans  van der  Pluijm  kufanya  usajili, hata  Lwandamina  licha  ya kuichukua  timu hiyo  katika  usajili  wa  mwezi Disemba 2016,  viongozi  wa  Yanga  walimpa  uhuru  na  kukubali  sajili  mbili  ambazo alizihitaji  ili kuongeza nguvu  katika  kikosi  kilichokuwa  chini  ya Hans.

Kiungo  wa  kati, Mzambia, Justine  Zulu  na yule  wa mashambulizi  Emmanuel Martin  walisajiliwa  mwezi  Disemba  na Lwandamina  ili kuongeza  hamasa,  ubora na  upana  wa kikosi  katika  nafasi  muhimu. Ukitazama  upana  wa kikosi  cha Yanga  hivi  sasa  unaweza kupata  matumaini.

Ally  Mustapha,Beno  Kakolanya  na Deo  Dida-hawa  ni magolikipa watatu  ambao  wanaweza  kuwa chaguo  la kwanza  katika  vikosi  vya timu nyingine. Juma Abdul, Ramadhani Kessy, Oscar  Joshua  na Mwinyi  Hajji  ni walinzi  wa pembeni ambao  yeyote  anayepata  nafasi  ya kucheza hutoa  huduma  inayotakiwa  na benchi  la ufundi.

Nahodha,Nadir  Haroub, Kelvin Yondan, Vicent  Bossou, Vicent  Andrew  na Pato Ngonyani  ni walinzi  watano  wenye  uwezo  mkubwa. Said Juma Makapu, Zulu, Mzimabwe  Thaban Kamusoko, Haruna  Niyonzima  na Juma  Mahadhi  hawa ni  viungo  wa  kati  wenye  uwezo  wa hali  ya  juu katika  soka  la Tanzania.

Deus  Kaseke, Geofrey Mwashuiya, Saimon Msuva  na Martin ni viungo  wanne  wa pembeni  ambao  wote  wanaweza  kufanya  vizuri  wakipewa  nafasi. Malimi Busungu, Mhilu, Matheo  Anthony,  Mrundi, Amis Tambwe, Mzimbabwe, Donald Ngoma na Mzambia, Obrey  Chirwa  ni  mastraika sita  ambao  wanaweza  kuisaidia  timu  kufunga  magoli.

Ukitazama kila nafasi  katika kikosi  hiki  ina wachezaji  wawili  wenye  uwezo usiopishana  sana hivyo  jambo  hilo  limekuwa  likimrahisishia  kocha  na wasaidizi  wake  kuwekeza  mbinu  zao  kwa usahihi  huku  wakiamini  hakuna tofauti kubwa  anapocheza  Mustapha, Beno au Dida, ama Kessy/Abdul.

Kikosi  kipana  chenye wachezaji  bora  waliosajiliwa na makocha wa timu kinaibeba Yanga kwa kiasi  kikubwa ndiyo  maana  licha  ya kutokuwepo kwa Ngoma bado Chirwa alifanikiwa kuibeba timu katika mchezo mgumu vs Mwadui FC wiki iliyopita.

Jambo  muhimu  ambalo  linapaswa  kupewa kipaumbele  kwa wachezaji  ni kujituma katika  viwanja vya  mazoezi  na kuwa tayari wakati wowote  kubeba  majukumu ya kuisaidia timu.

NGUVU YA WASHAMBULIAJI

Msuva  amekwishafunga  magoli  9 katika ligi kuu hadi  sasa, idadi  sawa  na magoli  yaliyofungwa na Tambwe. Ngoma na Chirwa wamefunga magoli 7  kila mmoja na Deus Kaseke  amekwisha funga magoli 6. Ukijumlisha  idadi  ya magoli  yaliyofungwa na wachezaji hao watano utapa  jumla ya magoli 38.

Ikiwa imefanikiwa kufunga  magoli 42 katika  michezo  20, magoli  38  kufungwa  na wachezaji  watano  ni ishara  kwamba  mambo  yanakwenda vizuri  kwa washambuliaji na mchango  wao  ni mkubwa sana  katika mafanikio  tarajiwa  ya timu yao.

Yanga ndiyo  timu iliyofunga  magoli mengi  msimu uliopita  na hadi sasa katika ligi ya msimu huu timu hiyo inaongoza kwa tofauti  ya magoli 12  zaidi  ya timu inayowafuatia katika ufungaji-Simba SC ambao wamefunga magoli 30.

Ili mafanikio yapatikane  ni lazima timu icheze  kwa uwiano  sawa  katika ulinzi, kiungo  na mashambulizi  na hili limeonekana wazi  kwa maana safu ya ulinzi inazuia  vizuri  ndiyo  maana wameruhusu magoli 9 tu.

Viungo wamekuwa wakitengeneza  nafasi nyingi  ndiyo  maana Msuva anaongoza  katika upigaji wa pasi  za mwisho akiwa ametengenezazaidi ya magoli kumi, Niyonzima na Kaseke pia wamehusika katika magoli   zaidi  ya kumi yaliyofungwa  na wachezaji wengine, huku washambuliaji wakijitahidi  kuhakikisha wanafunga magoli  ya kutosha kadri  itakavyowezekana.

UATAWALA

Achana  na  matatizo ambayo  yaliwahi  kuripotiwa  kuhusu  mishahara  ya wachezaji  na posho  zao kuchelewa mwezi Disemba hali iliyopelekea  kuangusha  pointi mbili vs African Lyon,  achana  na sababu  za wachezaji kulalamikia  mazoezi  ya kocha Lwandamina  wakati akianza kuifundisha timu hiyo mwezi Disemba, ukweli Yanga wametengeneza  timu moja  bora sana  katika  utawala.

Kumuajiri  aliyekuwa  mchezaji  mahiri wa  klabu na kocha Charles  Boniface Mkwassa katika  nafasi  ya  ukatibu  mkuu  wa  klabu  ni  jambo  jema  kwa klabu  na hata  benchi  la  ufundi na wachezaji. Uwepo  wa Hans  kama Mkurugenzi  wa Ufundi na  makocha Lwandamina, Mwambusi, Pondamali  na meneja Hafidh  Saleh  ni jambo  linaloongeza  hasama  kwa wachezaji.

Watu  hawa sita wakishirikiana vizuri  na uongozi  wa mwenyekiti Yusuph Manji  na makamu wake Clement Sanga  watazalisha  matokeo  chaya  kwa kiasi  kikubwa hadi  ndani  ya wachezaji.

Umoja, upendo, kuheshimiana na uwajibikaji unatakiwa katika timu hii  ya uongozi  kisha  wao  wanapaswa  kuwasambazia  wachezaji  wao pia. Nini  kitafuata? Ni  mafanikio  tu kwa sababu  watu  wa mpira  wamekutana  pamoja.

RATIBA

Katika  michezo  kumi iliyosalia  upande  wao, Yanga watasafiri  mara  mbili  tu  nje ya Dar es Salaam. Wataenda Morogoro  kucheza na Mtibwa Sugar  kisha watasafiri  kwenda Mwanza  kucheza na Mbao FC.

Michezo  mingine  minane  yote watacheza katika uwanja wa Taifa, Dar Es Salaam. Ratiba yao  wakiitumia vizuri  itawasaidia   kushinda  ubingwa  hasa  ukizingatia  wapinzani  wao  wa karibu watakuwa na michezo mingi nje  ya Dar.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 676

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>