Quantcast
Channel: Makala – ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 676

Kuna Messi Mmoja, Maradona Mmoja, na Dyabala Mmoja tu. Paulo Dyabala Na Ndoto Ya Baba Yake.

$
0
0

Kama ilivyokuwa kwa kila mtu nchini Italia, Paulo Dyabala aliathirika kwa kiasi kikubwa na balaa la Edoardo Di Carlo na Samuel Di Michelangelo, vijana wawili waliobaki yatima kutokana na maporomoko ya barafu maarufu kama Rigopiano yaliyotokea Januari 18 na kuchukua maisha ya watu 29.

Baada ya kusikia kuwa watu hao walikuwa mashabiki wa Juventus, Dyabala aliwapigia kwa njia ya video na kuwakaribisha Vinovo akiwa na imani kuwa atawaonyesha kuwa hawapo peke yao.

Stori zao hazikufanana nae lakini bado Dybala angeweza kufananisha hisia za hasara hiyo na upweke.

Akiwa na umri wa miaka 15, alimpoteza baba yake kutokana na saratani ya kongosho. Mdogo wa mwisho kati ya wavulana 3, ambaye ni Paulo hakushirikishwa na familia yake, akaachwa asijue lolote.

“Ili kunilinda hawakuniambia kila kitu”, aliweka wazi. “Nilikuwa nina imani atapata nafuu na kupona. Leo, ninamwota na ninaamka nikiwa mwenye machozi kila mara”.

Ukizingatia umuhimu aliokuwa nao baba yake na kifo chake, inaonyesha ni ajabu kwa namna ambayo Dyabala amefanikiwa kufika mbali hivi kwenye soka.

Hata hivyo, alikuwa ni Adolfo ambaye alikuwa ndiye msukumo kwenye kukomaa katika maisha ya soka ya mwanae. Wakati Paulo akienda kucheza soka katika klabu ya Newell Old Boys akiwa na miaka 8, baba yake hakuridhika na klabu hiyo. “Tutakaa nyumbani,” alimwambia mwanae.

Paulo hata hivyo alijiunga na Instituto de Cordoba and na ni baba yake aliyekuwa anamwendesha kwenda na kutoka mazoezini.

Baada ya Adolfo kufariki, Paulo hakuwa na namna zaidi ya kuondoka alikolelewa Laguna Larga na kwenda Cordoba, umbali wa saa moja kwa gari, na kuishi kwenye nyumba ya wageni ya klabu hiyo, hali iliyopelekea kupata jina la utani la ‘El pibe de la pensión’.

“Kilikuwa kipindi kigumu maishani mwangu, haikuwa rahisi,” alikiri Dybala huku akisema familia yake ilikuwa mbali sana.

“Nilikuwa najikuta nikijifungia bafuni na kulia sana. Lakini sikunyanyua mikono, sikufa moyyo.”

Ni kweli, Dyabala anasema kuwa kifo cha baba yake “kilimpa ngubu na kumjenga.” Hali iliyomkomaza na kumkuza.

Hili lilimfanya kuwa na malengo zaidi zaidi ya kipindi chochote akiamini atafanikiwa. “Baba yangu alikuwa na ndoto,” alielezea, “kuwa walau mmoja kati ya wanae aje kuwa mchezaji wa soka.

“Gustavo, ambaye ni mkubwa zaidi, hakufanikiwa lakini hata Mariano, ambaye kila mtu alisema alikuwa bora zaidi kuliko mimi lakini ambaye aliugua ugonjwa wakukumbuka nyumbani unaofahamika kama homesickness.

“Hivyo ilibidi nifanye hivyo ili kumtunza na kumpa heshima kwa kumbukumbu za baba yangu ambapo ningezifikia ndoto.”

Alifanya hivyo tu. Lakini miaka isiyozidi miwili baadae akiwa na umri wa miaka 17, Dybala  alikuwa mfungaji mdogo zaidi wa Cordoba  akivunja rekodi ya Mario Kempes.

Msimu uliofuata alifunga mabao 17 kwenye michezo 38 na ikamfanya apate jina linguine la utani, ‘La Joya’ (Kito), na akauzwa kwa kiasi cha Euro milioni 11.8 (€11.8) kwenda Parlemo.

Ilikuwa ni katika mji wa Sicily ambapo alikuja chini ya uangalizi wa Maurizio Zamparini. Wnaomfahamu Raisi wa zamani wa Palermo wanafahamu fika kuwa fikra zake inabidi zifikiriwe vyema, maneno yake yalibeba maana kubwa kama ilivyokuwa kwa mikataba aliyowapa makocha wake

Hivyo, pale ambapo Zamparini alipodai kuwa Dybala angekuwa mrithi wa Lionel Messi wakati akichomoza kwenye msimu wa 2014-15, wachache ambao hata walimtizama.

“Nilipomuuza kwenda Juventus kwa kiasi cha Euro milioni 32 (€32) ikiwemo na bonasi ya €8m, walilizungumzia hili kama jambo la ajabu,” Zamparini alikumbushia mapema mwaka huu.

“Sasa hivi wanasema Marotta ana akili za kipekee. Dybala ana thamani kiasi gani kwa sasa? Walau kiasi cha €100m; ni Messi mpya!”

Ni wazi wachezaji kama Gonzalo Higuain wamesema kuna ushabihiano: akili na mbinu za kukokota mpira, mgandamizo wa chini kutokana na kimo, aina ya kipekee ya kugusa mpira na mguu wa kushoto wa kipekee.

Lakini pia muhimu zaidi, Dybala anafanana na Messi katika kuamini kwa kiasi kikubwa kwenye uwezo wao.

Ilikuwa ni ajabu alipofika katika klabu ya Juventus hakuonyesha kushitushwa na mazingira mapya. Aliamini kuwa anastahili kuwepo kwenye moja ya vilabu vikubwa duniani.

Ni kweli, ikiwa Andrea Pirlo anaondoka katika msimu ule wa majira ya kiangazi, alichukua maamuzi ya kuwa anapiga mipira ya adhabu, akijaribu kufanana na Messi akiondolewa katika mchezo wa kwanza wa Argentina.

Hata hivyo kuendelea kufananishwa nap engine mchezaji bora wa muda wote ni msalaba mkubwa.

Gerard Deulofeu karibuni alikiri kuwa aliona ana mzigo mkubwa baada ya kupata nafasi ya kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha  Barcelona mwaka 2011.

Dybala, hata hivyo yupo tofauti, hawazi thamani atakayonunuliwa nayo, na wala hafanyi mambo kwa sababu anataka kuwa Messi mpya.

“Mimi ni Dyabala, nataka kuwa Dyabala pekee ingawa natambua kumekuwapo ufananisho. Kutakuwa na Messi mmoja tu, kama ilivyokuwepo Maradona mmoja.”

Ni wazi kuwa jambo pekee ambalo linaweza kuwa linamsumbua Dyabala ni kumuenzi baba yake. “Magoli yote ninayofunga ni zawadi kwake, soka limenisaidia sana na nimekuwa mchezaji kwa nguvu zake zaidi ya nguvu zangu.”

“Alinifunisha kupigana na kutokukubali kushindwa, ndoto yake ilikuwa kuniona uwanjani nikicheza. Najua leo baba ana furaha juu yangu.” Na hilo ndilo jambo ambalo Dyabala amekuwa akilihitaji siku zote

 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 676

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>